Kusoma alama za nyakati ni mojawapo ya vipengele muhimu kwa kila shirika la kimisionari. Kuhamishwa kwa shughuli za kiutawala kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma kama mji mkuu mpya, hakukuleta tu mabadiliko katika uwanja wa kisiasa wa Tanzania, bali pia katika Kanisa. Dodoma ilijikuta ikipokea wageni wengi kutoka maeneo mbalimbali ya nchi. Makanisa, shule, barabara na taasisi nyingine za kijamii ambazo hapo awali zilionekana kuwa za kutosha, zilijikuta hazitoshelezi kuhudumia idadi kubwa ya watu waliokuwa wakimiminika kutoka kila kona ya
Tanzania:
Soma Zaidi >>>