Abbey / Umisionari / Huduma kwa Wageni
UKARIMU KWA WAGENI ni kati ya tunu muhimu kabisa kwetu sisi Wabenediktini. Mt. Benedikto anatuagiza kuwapokea wageni wote kama vile tungempokea Kristu mwenyewe. Wote wanaotaka kututembelea, kusali na kushiriki utume wetu wanakaribishwa daima. Tunayo nyumba ya pekee kwa wageni wale ambao wangependa kufanya semina, mikutano, mafungo au kutulia kwa namna ya pekee. Tembelea tovuti hii kwa maelezo zaidi: zakeo.ndanda.org